ELCT Press Release

Date: February 5, 2019
Press release No. 001/02/2019

close window


Martin Junge Karibu Tanzania

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limemwalika Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa ya Kilutheri Duniani (FMKD), Mchg. Dkt. Martin Junge, kufanya ziara ya kichungaji ya siku nne nchini.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu wa KKKT, Bw. Brighton Killewa, imesema Mchg. Dkt. Junge atatoa mada kuu kuhusu: “Kujenga Jamii na Umoja wa Kanisa” kwenye faragha ya viongozi wa KKKT itakayofayika Wilayani Karatu kuanzia tarehe 20 hadi 22 Februari 2019.

Baada ya mazungumzo na uongozi wa Kanisa atatembelea Dayosisi ya Kaskazini kwa siku nzima ya tarehe 24 Februari 2019 ambapo ataanza kwa kushiriki na kuhubiri katika Ibada ya Jumapili Usharika wa Gezaulole Wilayani Hai na kutembelea baadhi ya vituo vya Dayosisi vilivyoko Wilaya ya Hai, Kilimanjaro.

Katibu Mkuu huyo wa FMKD atawasili Tanzania tarehe 20 Februari 2019 na anatarajiwa kurudi Geneva, Uswisi tarehe 24.

Bw. Killewa alisema faragha hiyo ya viongozi itahudhuriwa na watu 41 wakiwemo maaskaofu wa KKKT. Mada mbalimbali zitatolewa na kujadiliwa wakati wa warsha iliyoandaliwa kwenye faragha hiyo.

ELCT welcomes Martin Junge

The Evangelical Lutheran Church in Tanzania (ELCT) has invited the General Secretary of the Lutheran World Federation, Rev. Dr. Martin Jungefor a four-day pastoral visit to Tanzania.

A statement issued today by the ELCT Secretary General , Mr. Brighton Killewa, said that Dr. Junge will deliver a keynote address on: “Communion Building and Church Unity” during ELCT Church leaders retreat due to take place 20 – 22 February 2019.

Among other things, after carrying out discussions with the ELCT leadership, he will pay a one-day visit to Northern Diocese on 24 February 2019 starting with delivering of a sermon at a Sunday Worship Service at Gezaulole Lutheran Parish (Hai District) as well as tour some institutions run by the diocese in Hai District, Kilimanjaro Region.

The LWF General Secretary arrives in Tanzania on 20th February and is expected to return to Geneva, Switzerland on the 24th February.

Mr Killewa said 41 people will attend the leadership retreat, including ELCT bishops. A number of papers will be presented and discussed during a workshop as part of the retreat.

 


Mchg. Dkt. Martin Junge,
Katibu Mkuu wa Fungamano la Makanisa Kanisa Duniani.


Elizabeth Lobulu
Communication Coordinator,
Evangelical Lutheran Church in Tanzania
Box 3033, ARUSHA, Tanzania.
Phone: +255-27-250-8856/7
FAX: +255-27-254-8858
E-mail: ELobulu@elct.or.tz

Close this window

For more information contact:

Elizabeth Lobulu
Communication Desk Officer, ELCT
E-mail: ELobulu@elct.or.tz